SOMO LA USIKU,.
YAFAHAMU MAANDIKO.
SOMO :POKEA SILAHA ILI ZIKULINDE USIKU HUU
FUNGU KUU: ISAYA 54:17
17 Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.
Mpendwa hebu tafakari juu ya URITHI NA HAKI kwa watumishi wa Mungu ulivyo wa ajabu;
1.Kila silaha
itakayofanyika juu yangu HAITAFANIKIWA
2.Kila ulimi
utakaoinuka juu
yangu katika hukumu
NITAUHUKUMU KUWA mkosa.
Mpendwa ni haki yako kama mtumishi wa Bwana kupata ulinzi wa Ki Mungu katika mazingira yote.
Ulimi unaumba jambo zuri au baya. Ulimi unaotamka baya juu yangu hauna nafasi kwa jina la Yesu.
Mungu akubariki sana, simama katika neno upokee ushindi dhidi ya silaha zote zinazorushwa juu yako.
UWE NA USIKU MWEMA MTU WA MUNGU
Imeandaliwa na mwandishi wako
Maoni
Chapisha Maoni
THANKS FOR COMMENTING
Name:
Where are you comming from:
Mobile no.:
Comment: